Friday, February 21, 2014

NEUER AMKUNA RAIS WA BAYERN.

RAIS wa klabu ya Bayern Munich, Uli Hoeness ameonyesha kumhusudu Manuel Neuer kutokana na kiwango bora alichoonyesha katika ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Arsenal katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya uliochezwa Jumatano. Golikipa huyo wa kimataifa wa Ujerumani alifanikiwa kupangua penati iliyopigwa na Mesut Ozil mapema katika mchezo huo pamoja na kuokoa michomo kadhaa kutoka kwa wapinzani wao iliyowezesha kuiweka timu hiyo sawa. Akihojiwa Hoeness amesema golikipa huyo amekuwa katika kiwango chake cha juu kabisa na haoni kama anaweza kuuzika kwa bei yoyote. Mbali ya kuokoa michomo hatari lakini pia Neuer amekuwa mazuri kwa kusaidia wachezaji wenzake kwa pasi zake za ufundi huku akiweza kutumia miguu yake yote miwili kwa ustadi. Neuer hajafungwa mechi 22 kati ya 35 alizocheza na Bayern msimu huu 2013-2014.

No comments:

Post a Comment