Friday, February 21, 2014

ROBBEN KUSAINI MKATABA MPYA UTAKAOMUWEKA ALLIANZ ARENA MPAKA 2017.

WINGA mahiri wa klabu ya Bayern Munich, Arjen Robben amefikia makubaliano juu ya mkataba mpya ambao utamuweka klabuni hapo mpaka 2017. Nyota huyo wa kimataifa wa Uholanzi mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika majira ya kiangazi mwaka 2015 na pande zote mbili zimekuwa katika mazungumzo katika wiki kadhaa. Hivi karibuni Robben alielezea uhakika wake wa kuendelea kubakia Bayern na kubainisha kuwa kilichobaki kufanya sasa ni kukamilisha taratibu za kusaini makaratasi. Robben amesema kuwa kilichobakia ni kutia saini mkataba wake mpya lakini kuna mambo yanayoendelea hivi sasa ikiwemo michezo mingi na kusafiri ndio maana anaweza kuchelewa kidogo kusaini mkataba huo. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 30 alijunga na Bayern akitokea Real Madrid mwaka 2009 na toka kipindi hicho amekuwa mchezaji muhimu wa mabingwa hao wa Ujerumani na Ulaya akiwa ametupia nyavuni mabao saba katika mechi 16 za Bundesliga alizocheza msimu huu.

No comments:

Post a Comment