Wednesday, February 26, 2014

TULISTAHILI KUFUNGWA - MOYES.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, David Moyes amekiri kikosi chake kucheza kwa kiwango kibovu zaidi msimu huu katika michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Olympiakos. Mabao yaliyofungwa katika kila kipindi na Alejandro Dominguez na Joel Campbell yaliwahakikishia ushindi mabingwa hao wa Ugiriki na kuiacha United katika wakati mgumu wa kufuzu robo fainali ya michuano hiyo. Kikosi cha Moyes kilifanikiwa kupiga shuti moja pekee langoni mwa wapinzani wao kwenye mchezo huo na kocha huyo Mscotland anakiri wachezaji walistahili kufungwa mechi hiyo. Moyes amesema wachezaji wake walicheza kwa kiwango kibovu sana na kitu kizuri pekee ni kwasababu wana mchezo wa pili wa kujiuliza. Michuano hiyo inaendelea tena leo ambapo Chelsea watakuwa wageni wa Galatasaray jijini Istanbul, Uturuki huku Wajerumani Schalke 04 wakiwakaribisha Real Madrid.

No comments:

Post a Comment