Wednesday, February 26, 2014

KESI YA PISTORIUS KUONYESHWA MOJA KWA MOJA KATIKA LUNINGA.

JAJI Dunstan Mlambo wa mahakama ya Pretoria nchini Afrika Kusini anayesikiliza kesi ya mwanariadha mlemavu Oscar Pistorius ameruhusu kesi hiyo kuonyesha moja kwa moja katika luninga pindi itakapoanza kusikilizwa. Pistorius anakabiliwa na kesi ya kumuua kwa kumpiga risasi mpenzi wake ambaye ni mwanamitindo na mtangazaji Reeva Steenkamp zaidi ya mwaka mmoja uliopita. Waendesha mashtaka wanamtuhumu Pistorius kufanya mauaji hayo kwa kukusudia lakini mwenyewe alikana akidai kuwa alifanya mauaji hayo kwa bahati mbaya akidhani kuwa alivamiwa na majambazi. Mwandishi wa BBC Pumza Fihlani amesema hiyo itakuwa mara ya kwanza kwa kesi nchini humo kusikilizwa huku ikirushwa moja kwa moja katika luninga.

No comments:

Post a Comment