Wednesday, February 26, 2014

MASHABIKI WA CHELSEA WARIPOTIWA KUSHAMBULIWA ISTANBUL.

WAKATI imebaki saa chache kabla ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kati ya Galatasaray na Chelsea kumekuwa na ripoti kuwa baadhi ya mashabiki wa timu hiyo ya Uingereza wameshambuliwa jijini Istanbul. Shabiki mmoja ameripotiwa kuchomwa kisu mguuni na mwingine kupigwa karibu na eneo la Taksim Square lililopo katikati ya mji huo ambapo mashabiki wawili wa Leeds United walishambuliwa na kuuawa mwaka 2000 kuelekea katika nusu fainali ya mchezo wa Kombe la UEFA. Taarifa hiyo haikusema kama majeruhi hao walilazwa hospitalini lakini klabu imeshaonywa kuhusiana na tukio hilo. Ofisa wa mambo ya nje alithibitisha kufanyia uchunguzi taarifa hiyo na watachukua hatua stahiki itakapothibitika kutokea kwa tukio hilo.

No comments:

Post a Comment