Wednesday, February 26, 2014

CARLOS ATAMANI KUINOA MADRID.

BEKI nguli wa zamani wa klabu ya Real Madrid, Roberto Carlos amekiri kuwa angependa kuinoa klabu hiyo ndani ya miaka kumi ijayo. Nyota huyo wa kimataifa wa Brazil ametumia miaka 11 Santiago Bernabeu akiwa kama mchezaji na kuisaidia timu hiyo kushinda mataji manne ya La Liga na matatu ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Carlos mwenye umri wa miaka 40 kwasasa ni kocha wa timu ya Sivasspor ya Uturuki. Carlos alikaririwa na gazeti la Marca la Hispania akidai kuwa kuinoa Madrid ndani ya kipindi cha miaka 10 ijayo ni moja ya ndoto zake kwa hivi sasa.

No comments:

Post a Comment