Wednesday, February 26, 2014

CAMPBELL APANIA KUREJEA ARSENAL.


MCHEZAJI chipukizi anayecheza kwa mkopo katika timu ya Olympiakos, Joel Campbell amesisitiza kuwa anataka kuonyesha thamani kwa Arsene Wenger na kupambana ili aweze kurejea katika timu yake ya Arsenal msimu ujao. Kinda huyo wa kimataifa wa Costa Rica alisaini mkataba wa miaka mitatu na Arsenal lakini ametumia muda wake mwingi katika mkataba huo akicheza kwa mkopo huku pia akikosa kibali kitakachomuwezesha kusakata kabumbu Uingereza. Campbell mwenye umri wa miaka 21 ameonyesha kiwango kizuri msimu huu akiwa na Olympiakos huku akifunga moja ya mabao katika ushindi wa mabao 2-0 waliopata dhidi ya mabingwa wa Ligi Kuu Manchester United katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Campbell amesema Arsenal walipomfuata hakusita kujiunga nao na anaamini hivi sasa tayari ameiva kuichezea klabu hiyo msimu ujao.

No comments:

Post a Comment