Monday, February 24, 2014

WAHUNI WA GALATASARAY NA BESIKTAS WACHAPANA KAVU KAVU MTAANI.

IKIWA imebaki siku chache kabla ya Galatasaray kuikaribisha Chelsea katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya, kumezuka vurugu za kupigana na kurushiana viti kati ya mashabiki wa Galatasaray na mahasimu wao Besiktas katika mitaa ya jiji la Istanbul. Kumekuwa na picha za video katika mtandao wa Youtube ukionyesha makundi makubwa ya wahuni wa Galatasaray na Besiktas wakichapana katika mitaa yenye maduka mengi kabla ya mchezo baina ya timu hizo katika Uwanja wa Turk Telekom. 
Vurugu hizo ziliendelea pia wakati wa mchezo huo ambao Galatasaray ilishinda kwa bao 1-0. Mashabiki wa Chelsea watakaosafiri kwenda jijini Istanbul kwa ajili ya kuishangilia timu yao wameonywa kuwa makini pindi watakapokuwa huko.


No comments:

Post a Comment