Monday, February 24, 2014

MOURINHO AMTAMANI FALCAO KWA UDI NA UVUMBA.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amedokeza kuwa anaweza kumsajili mshambuliaji wa Monaco, Radamel Falcao katika usajili wa majira kiangazi. Mourinho ameshindwa kuficha hisia zake za kumtamani nyota huyo ambaye kwasasa yuko benchi akiuguzi goti lake na kuna ripoti kuwa anafikiria kuondoka Ufaransa baada ya kucheza kwa mwaka mmoja kutokana na Ligi Kuu ya nchi hiyo kukosa ushindani. Akihojiwa Mourinho pia aliondoa uwezekano wa kuhitaji huduma ya washambuliaji wa timu ya Paris Saint-Germain Zlatan Ibrahimovic na Edinson Cavani. Mourinho amesema ana timu lakini hana mshambuliaji na Falcao ni kama hana timu kwasababu mchezaji wa kiwango kama chake hastahili kucheza mbeke ya mashabiki 3,000. Mourinho alienda mbali na kudai kuwa Monaco ni klabu ambayo mchezaji anaweza kumalizia soka lake wakati akiwa ameanza kuchuja. Falcao mwenye umri wa miaka 28 alijiunga na Monaco kwa paundi milioni 50 akitokea Atletico Madrid katika majira ya kiangazi mwaka jana.

No comments:

Post a Comment