Monday, February 24, 2014

RAMSEY AACHWA KIKOSI CHA WALES.

TIMU ya taifa ya Wales itamkosa kiungo wake mahiri Aaron Ramsey wakati watakapocheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Iceland Machi 5 mwaka huu. Kiungo huyo wa Arsenal mwenye umri wa miaka 23 bado anajiuguza baada ya kupata majeraha ya msuli Desemba mwaka jana. Wakati Ramsey akishindwa kujumishwa katika kikosi cha nchi hiyo kocha Chris Coleman amemuita winga wa Real Madrid Gareth Bale katika kikosi chake ambacho kitacheza mechi hiyo katika Uwanja wa Cardiff City. Coleman pia amemuita kinda wa Manchester City Emyr Huws ambaye kwasasa anacheza kwa mkopo katika timu ya Birmingham City na kuna uwezekano kinda huyo mwenye miaka 20 akapata nafasi ya kucheza mechi yake ya kwanza katika timu ya wakubwa ya nchi hiyo. Mchezo dhidi ya Iceland utakuwa muhimu kwa Wales kujenga kikosi chake tayari kwa mechi za kufuzu michuano ya Ulaya 2016 ambapo wamepangwa katika kundi B sambamba na Ubelgiji, Bosnia-Hercegovina, Israel, Cyprus na Andora.

No comments:

Post a Comment