Monday, February 24, 2014

PIRLO ASISITIZA KUBAKIA JUVENTUS.

KIUNGO mkongwe Andrea Pirlo amesisitiza kuwa hajafanya mawasiliano yoyote na Real Madrid kuhusu suala la uhamisho katika majira ya kiangazi na amepanga kuendelea kubakia Juventus. Nyota huyo wa kimataifa wa Italia mkataba wake na Juventus unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu na Madrid wanamfuatilia kwa karibu mkongwe huyo. Hata hivyo Pirlo amesema kwasasa akili yake iko vibibi hivyo vya Turin na anategemea kufikia makubaliano juu ya nyongeza ya mkataba wake mapema iwezekanavyo. Pirlo amesema hajawahi kuzungumza na Madrid kuhusu uhamisho lakini amekiri mara kadhaa amekuwa akizungumza na Carlo Ancelotti kuhusu mambo mengine. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 34 amesema anajisikia vyema kuendelea kuwepo Juventus hivyo hana mpango wa kwenda popote kwasasa.

No comments:

Post a Comment