Monday, February 24, 2014

VAN GAAL BADO AITAMANI SPURS.

KWA mara nyingine kocha wa timu ya taifa ya Uholanzi, Louis van Gaal amegusia uwezekano wake wa kuhamia Ligi Kuu nchini Uingereza kuifundisha Tottenham Hotspurs baada ya michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Brazil. Spurs wamejipanga kuanza mazungumzo mapya na Van Gaal kuhusu kuinoa klabu hiyo baada ya michuano hiyo itakayofanyika baadae mwaka huu. Mkataba wa Van Gaal na Uholanzi unatarajiwa kumalizika baada ya Kombe la Dunia na ameonekana hana mpango wa kuongeza mwingine. Akihojiwa Van Gaal mara baada ya droo ya ratiba ya kufuzu michuano ya Ulaya 2016, amesema hata kuwa kocha wa timu hiyo wakati wakianza kampeni zao na hajui ataelekea wapi baada ya hapo lakini kama akipata changamoto mpya hatasita kuichukua. Van Gaal amesema changamoto mpya atakayochukua ni kufundisha timu ya Ligi Kuu nchini Uingereza na inawezekana ikawa Spurs lakini kwasasa anaangalia safari yao ya Brazil.

No comments:

Post a Comment