Monday, February 24, 2014

NASRI AJISTUKIA KUWA NA GUNDU.

KIUNGO wa klabu ya Manchester City, Samir Nasri ana hofu kuwa wakifungwa katika mchezo wa fainali ya Kombe la Ligi wiki ijayo inaweza kuwaathiri katika kampeni zao wa kuwania taji la Ligi Kuu kama ilivyokuwa kwa Arsenal. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa alifika fainali ya michuano hiyo akiwa na Arsenal mwaka 2011 lakini walipata kipigo cha kushtusha kutoka Birmigham ambao walikuwa wanashuka daraja msimu huo. Kipigo hicho kiliichanganya Arsenal na kujikuta wakishinda mechi mbili kati ya 11 walizocheza za Ligi na kuporomoka kutoka nafasi ya pili mpaka ya nne mwishoni mwa msimu wakimaliza kwa tofauti ya alama 18 na mabingwa Manchester United msimu huo. Nasri pia alikuwa sehemu ya kikosi cha City kilichochapwa na Wigan katika mchezo wa fainali ya Kombe la FA msimu uliopita na nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 amepania kuhakikisha timu yake inaibuka kidedea ili yasije kuwakuta yalioikuta Arsenal. Akihojiwa Nasri alikiri kuwa hana kumbukumbu nzuri na vikombe baada ya kupoteza fainali akiwa na Arsenal na pia City msimu uliopita hivyo hataki suala hilo lijirudie tena.

No comments:

Post a Comment