Monday, February 24, 2014

DAVIDS AMVULIA KOFIA CONTE.

MCHEZAJI wa zamani wa kimataifa wa Uholanzi, Edgar Davids ameeleza jinsi anavyomkubali kocha wa Juventus Antonio Conte na anaamini kuwa angepata wakati mgumu hata kuwepo katika mechi la wachezaji wa akiba kutokana na jinsi mabingwa hao wa Serie A walivyokuwa imara. Davids aliichezea Juventus kati ya mwaka 1997 na 2004 na kufanikiwa kushinda mataji matatu ya Serie A na timu hiyo huku pia akifanikiwa kutinga fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya msimu wa 2002-2003. Nguli huyo aliuambia mtandao wa klabu hiyo kuwa kiwango cha timu hiyo kwasasa kiko juu kiasi ambacho angekuwa bado anacheza hadhani kama angeweza kuwemo katika benchi la wachezaji wa akiba. Davids amesema kwasasa Juventus wana kikosi kizuri wakiwemo wachezaji kama Arturo Vidal na Paul Pogba ambao wametoa mchango mkubwa msimu huu. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 40 pia alimpongeza Carlos Tevez kwa kuongeza chachu ya ushindi katika safu ya ushambuliaji akiwa mefunga mabao 14 katika mechi 25 za Serie A alizocheza msimu huu.

No comments:

Post a Comment