Monday, February 24, 2014

NADAL ANYAKUWA TAJI LA RIO OPEN.

NYOTA wa tenisi kutoka Hispania, Rafael Nadal amefanikiwa kumgaragaza Alexandr Dolgopolov wa Ukraine kwa 6-3 7-6 na kunyakuwa taji la michuano ya wazi ya Rio de Janeiro nchini Brazil. Ushindi huo wa Nadal ambaye anashika nafasi ya kwanza katika orodha za ubora duniani umekuja ikiwa zimepita wiki nne baada ya kupoteza taji la michuano ya wazi ya Australia kwa Stanislas Wawrinka. Katika mchezo huo Nadal ambaye aliumia mgongo wakati wa mazoezi katika michuano ya Melbourne hakuonyesha kutetereshwa na mpinzani hivyo kuonyesha dalili kuwa amepona. Hilo linakuwa taji la 43 kwa Nadal katika viwanja vya udongo na pia hajawahi kupoteza mchezo katika viwanja hivyo toka alipochapwa na Novak Djokovic katika michuano ya Monte Carlo Masters miezi 10 iliyopita.

No comments:

Post a Comment