Wednesday, February 26, 2014

ZLATAN NI MMOJA YA WACHEZAJI WATATU BORA DUNIANI - BECKHAM.


NGULI wa soka David Beckham amemtaja mshambuliaji wa Paris Saint-Germain Zlatan Ibrahimovic kama mmoja ya wachezaji ambao amepata kucheza nao na kumuweka katika orodha ya wachezaji watatu bora duniani. Beckham ambaye ni nahodha wa zamani wa Uingereza alimalizia soka lake PSG msimu uliopita na kukisaidia kikosi hicho kilichokuwa kikinolewa na Carlo Ancelotti wakati huo kunyakuwa taji la Ligi Kuu nchini Ufaransa baada ya kusaini kuitumikia klabu hiyo Januari. Beckham ambaye amecheza na nyota wengine kama Zinedine Zidane na Ronaldo wakati wa enzi zake anaamini Msweden huyo ni mmoja wa wachezaji bora katika soka kwasasa. Akihojiwa Beckham amesema kucheza timu moja Ibrahimovic ilikuwa ni jambo la kipekee kwasababu ni mmoja ya wachezaji wenye vipaji aliopata kuwaona wakati akicheza soka. Ibrahimovic amefunga jumla ya mabao 37 katika mashinano yote msimu huu.

No comments:

Post a Comment