Wednesday, February 26, 2014

NGULI WA ZAMANI WA BENFICA NA NAHODHA URENO KUFANYIWA MAZISHI YA KITAIFA MSUMBIJI.

MSUMBIJI inatarajia kumfanyia mazishi ya kitaifa mchezaji wa zamani wa Benfica na nahodha wa Ureno Mario Coluna ambaye amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 78. Coluna aliisaidia Benfica kushinda taji la Ulaya mara mbili huku akiiongoza Ureno akiwa nahodha kushika nafasi ya tatu katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 1966. Mwishoni mwa maisha ya uchezaji, Coluna alirejea Msumbiji ambako alizaliwa na akaifundisha timu ya taifa ya nchi hiyo kwa muda. Coluna pia aliwahi kuliongoza Shirikisho la Soka la Msumbiji na pia waziri wa michezo wan chi hiyo. Rais wa klabu ya Benfica, Luis Felipe Vieira alituma salamu zake za rambirambi kwa msiba wa nguli huyo. Coluna alizaliwa Msumbiji mwaka 1935 na kuanza kucheza soka jijini Maputo kabla ya kusaini Benfica mwaka 1954 na kuifungia mabao 150 katika mechi 677 alizocheza.

No comments:

Post a Comment