Thursday, February 27, 2014

FARAH, BOLT, RONALDO, NADAL, VETTEL KUSHINDANIA TUZO YA MWANAMICHEZO BORA WA MWAKA.

MWANARIADHA nyota wa Uingereza Mo Farah ambaye ni bingwa wa mashindano ya dunia katika mbio za mita 5,000 na 10,000 yaliyofanyika jijini Moscow, Urusi mwaka jana, ametajwa katika orodha ya wanamichezo watakaogombea tuzo ya dunia ya mwanamichezo bora wa mwaka. Mbali na Farah wanamichezo wengine waliopo katika orodha hiyo ni pamoja na bingwa wa dunia wa mashindano ya langalanga Sebastian Vettel, nyota wa tenisi Rafael Nadal, mwanasoka Cristiano Ronaldo na nyota wa mpira wa kikapu wa Marekani LeBron James. Mwanariadha nyota wa mbio fupi kutoka Jamaica, Usain Bolt ambaye amewahi kushinda tuzo hiyo mara tatu naye pia ameteuliwa katika orodha hiyo kwa mara nyingine. Sherehe za utoaji wa tuzo zinatarajiwa kufanyika jijini Kuala Lumpur, Malysia Machi 26 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment