Thursday, February 27, 2014

MOYES ATAMBA KUWA WALISTAHILI KUSHINDA.

MENEJA wa klabu ya Galatasaray, Roberto Mancini anafikiri kuwa Chelsea walistahili kufungwa na timu yake katika mchezo wao wa mkondo wa kwanza wa Ligi ya Mabibgwa barani Ulaya hatua ya timu 16 bora uliochezwa jana. Juhudi za Chelsea kuanza mchezo huo kwa kasi zilizaa matunda baada ya kupata bao la mapema la dakika ya tisa kupitia kwa Fernando Torres lakini Galatasaray walionyesha kutawala mchezo huo kwa kipindi kirefu. Wenyeji Galatasaray walifanikiwa kurudisha bao hilo mapema katika kipindi cha pili kupitia kwa Aurelien Chedjou na kupelekea mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa Turk Telekom Arena kumalizika kwa sare ya bao 1-1. Akihojiwa Mancini amesema hakuridhishwa na matokeo hayo kwasababu anadhani kipindi cha pili walistahili kupata bao lingine zaidi ambao lingewafanya kuibuka na ushindi. Chelsea wanatarajiwa kuikaribisha Galatasaray katika mchezo wa mkondo wa pili utakaochezwa Machi 18 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment