Thursday, February 27, 2014

MOURINHO AMZUSHIA BALAA ETO'O KUHUSU UMRI WAKE.

SUALA la umri mkubwa kwa mshambuliaji wa Chelsea, Cameroon Samuel Eto'o limechukua sura mpya baada ya mpenzi wa zamani kujitokeza na kushindilia msumari mwingine. Meneja wa Chelsea Jose Mourinho alikaririwa na moja ya vyombo vya habari vya nchini Ufaransa akisema tatizo la timu yake ni safu ya washambuliaji ambao wamekuwa butu kwakuwa wana umri tofauti na ule unaofahamika. Mourinho alimtolea mfano Eto’o akidai kuwa ana miaka 32 lakini inawezekana ana miaka mitatu zaidi ya hiyo ambayo inatajwa ingawa baadae alipinga kauli yake hiyo na kudai alizungumza kiutani na mtu ambaye hajui mpira huku wakicheka lakini akashangaa kupelekwa kwenye vyombo vya habari. Sasa kama hiyo haitoshi mpenzi wake wa zamani na mama wa mtoto wake wa kwanza Anna Barranca mwenye umri wa miaka 43 amesema ana ushahidi kuwa mshambuliaji huyo ana miaka zaidi ya aliyotaja wakati anaingia barani Ulaya na anadhani hana miaka 35 ana miaka zaidi ya 39. Mwanamama huyo amesema Eto’o amezaliwa mwaka 1974 ambayo inamfanya awe ana miaka 39 kwasasa lakini hati yake ya kusafiria inaonesha kuwa ana miaka 32. Akiulizwa kuhusiana na suala la umri wake Eto’o mwenyewe hakutaka kulizungumzia na kudai kuwa siku zote amekuwa mkweli kwa timu anazocheza na kitu pekee anachotaka ni kuisaidia Chelsea kushinda mataji.

No comments:

Post a Comment