Thursday, February 27, 2014

MURRAY ATINGA ROBO FAINALI ACAPULCO.

MCHEZAJI nyota wa Uingereza, Andy Murray amefanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya michuano wazi ya Mexico kwa ushindi wa 6-3 6-4 dhidi ya Joao Sousa waa Ureno katika mchezo uliochezwa jijini Acapulco. Murray ambaye kama akishinda mchezo wake wa robo fainali atakuweza kucheza nusu fainali yake ya kwanza kwa mwaka huu anatarajiw akupambana na Gilles Simon wa Ufaransa. Katika mechi zingine zilizochezwa David Ferrer alifanikiwa kumtandika Mhispania mwenzake Feliciano Lopez kwa 7-6 6-2 huku Grigor Dimitrov akimuondosha Marcos Baghdatis kwa 6-1 6-4. Murray atapambana na Sousa anayeshika nafasi ya 23 huku akiwa na rekodi nzuri ya kushinda mechi 11-1 walipokutana kipindi cha nyuma.

No comments:

Post a Comment