Wednesday, March 26, 2014

MASHABIKI WAMGEUKA FERGUSON KWA KUWACHAGULIA BOMU MOYES.

MASHABIKI wa klabu ya Manchester United wamemgeukia kocha wa zamani wa timu hiyo Sir Alex Ferguson baada ya kuona wakipokea kipigo kutoka mahasimu wao Manchester City katika Uwanja wa Old Trafford jana usiku. City ambao waliwasambaratisha majirani zao hao kwa mabao 3-0 yaliyofungwa na Edin Dzeko na Yaya Toure, waliamsha hasira kwa mashabiki hao na kuanza kuonyesha mabango ya kumlaumu Ferguson ambaye ndiye aliyemchagua David Moyes kuchukua nafasi yake. Mbali na kumshambulia Ferguson lakini pia kulikuwa mabango mbalimbali ya kumpinga Moyes kwenye mchezo huo. Hasira za mashabiki hao zimeibuka kutokana na timu hiyo kushindwa kufanya vyema msimu huu hususani katika uwanja wao wa nyumbani.

No comments:

Post a Comment