Wednesday, March 26, 2014

MAJERUHI NDIO WANAONIKWAMISHA - WENGER.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amebainisha kuwa Aaron Ramsey amebakisha wiki mbili kabla ya kurejea tena uwanjani na kukiri kuwa ni ngumu kupambana huku wachezaji wako nyota wakiwa majeruhi. Kiungo wa kimataifa wa Wales mara mwisho kuvaa jezi ilikuwa ni Desemba 26 mwaka jana ambapo alishindwa kurejea uwanja mara mbili baada ya majeruhi yaliyokuwa yakimsumbua kumrudia. Sasa Wenger amesema kiungo huyo amebakisha muda kidogo kabla ya kurejea uwanjani wakati Mesut Ozil, Jack Wilshere na Laurent Koscielny pia wakiendelea kujiuguza. Akizungumza baada ya sare ya mabao 2-2 dhidi ya Swansea City, Wenger amesema ni jambo ngumu kupambana huku nusu ya wachezaji wako tegemeo wakiwa majeruhi.

No comments:

Post a Comment