Monday, March 3, 2014

MOYES ANAHITAJI MUDA - FERGUSON.

KLABU ya Manchester United imekua ikisuasua katika msimu wake wa kwanza bila kocha wake wa zamani Sir Alex Ferguson huku kocha mpya wa klabu hiyo David Moyes akiwa na hatihati ya kushindwa kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya. Pamoja na mwenendo mbaya wa timu hiyo ambao umepelekea mashabiki wengi kukiri kuwa Moyes hakustahili kibarua hicho hali ni tofauti kwa Ferguson ambaye anaamini kuwa kuyumba katika msimu wa kwanza ni jambo la kawaida. Akihojiwa wakati wa utoaji tuzo za filamu za Oscar huko jijini Los Angeles, Marekani kocha huyo mstaafu mwenye umri wa miaka 72 amesema hana shaka kwamba timu itakuja kubadilika na kwasasa sasa hivi ni mapema sana na kuna mambo mengi yamebadilika. Ferguson aliendelea kudai kuwa Moyes anahitaji muda kwani ameinoa klabu hiyo kwa miaka 27 hivyo kuja kwa meneja mpya itachukua muda kidogo lakini watarudi katika hali yao ya kawaida. Kocha huyo amejiwekea heshima ya kuwa kocha mwenye mafanikio zaidi katika soka nchini Uingereza katika miaka yake 27 aliyokaa Old Trafford ambapo alifanikiwa kunyakuwa mataji 13 ya Ligi Kuu na mawili ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya.

No comments:

Post a Comment