Saturday, March 22, 2014

NAUJUA UDHAIFU WA BAYERN HIVYO MSIWE NA HOFU - MOYES.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, David Moyes amesema ameshagundua udhaifu wa mchezo wa Bayern Munich na atajaribu kuutumia ili wakati timu hizo zitakapokutana katika hatua ya robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya. United wamepangwa na mabingwa hao watetezi katika ratiba iliyopangwa Ijumaa baada ya kuizabua Olympiakos na kutinga hatua hiyo. Bayern kwasasa wako kileleni mwa msimamo wa Bundesliga kwa tofauti ya alama 23 huku wakiwa wamecheza mechi 50 bila kufungwa lakini Moyes bado anaamini United inayoweza kupata matokeo katika mchezo huo. Moyes amesema amejaribu kuchukua vitu vichache kwa ajili ya kuvifanyia kazi ambavyo anaamini ndio udhaifu wa Bayern walionao na ni mategemeo yake vinaweza kusaidia.

No comments:

Post a Comment