Wednesday, March 26, 2014

SAGNA AKATAA KUJIUNGA NA INTER.

RAIS wa klabu ya Inter Milan, Erick Thohir amethibitisha kuwa beki wa klabu ya Arsenal Bacary Sagna amekataa ofa ya kujiunga nao. Mkataba wa Sagna unamalizika katika majira ya kiangazi na tayari imebainika kuwa Arsenal wamempa ofa ya mkataba wa miaka miwili ambao utamfanya kulipwa kitita cha paundi 75,000 kwa wiki. Inter walikuwa na mategemeo ya kumshawishi beki huyo wa kimataifa wa Ufaransa kuikacha klabu hiyo na kwenda nchini Italia lakini Thohir sasa amebainisha mpango hautawezekana kutokana na Sagna kukataa. Thohir aliwaambia waandishi wa habari kuwa Sagna ameamua kubakia Ligi Kuu ya Uingereza lakini bado wataendelea na mpango wao wa kuimarisha safu yao ya ulinzi.

No comments:

Post a Comment