Wednesday, April 23, 2014

BAADA YA KUKAA NJE KWA MIEZI 13 HATIMAYE DIABY AREJEA TENA UWANJANI.

KIUNGO Abou Diaby amerejea uwanjani kwa mara ya kwanza baada ya kukaa nje kwa zaidi ya mwaka wakati alipocheza kwa dakika 45 katika kikosi cha Arsenal cha vijana chini ya mri wa miaka 21 waliocheza na Chelsea. Mara ya mwisho kiungo huyo mwenye umri wa miaka 27 kuonekana uwanjani ilikuwa ni Machi 27 mwaka jana katika mchezo dhidi ya Swansea City ambapo aliumia msuli wa ndani ya goti. Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amedokeza kuwa kurejea uwanjani kwa nyota huyo kunaweza kuwa dalili njema za kurejea katika kikosi cha kwanza. Wenger amesema Diaby hajacheza soka kwa kipindi cha mwaka mzima lakini kimwili yuko tayari kucheza, kwasasa ni suala la maamuzi na anahitaji mechi nyingi zaidi ili aweze kuzoea changamoto kwa tena.

No comments:

Post a Comment