Wednesday, April 23, 2014

MOURINHO KUWAPUMZISHA NYOTA WAKE KATIKA MCHEZO DHIDI YA LIVERPOOL.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amesema anataka kuwapumzisha nyota wake kwa ajili ya safari kwenda Anfield kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Liverpool Jumapili ijayo. Chelsea bado bado wako katika kinyang’anyiro cha taji la ligi wakiwa wamebakiwa na michezo mitatu lakini Mourinho anataka kuhamishia nguvu zake katika mchezo wa marudiano wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Atletico Madrid. Hata hivyo, kocha huyo amesema uamuzi huyo wa kuwapumzisha baadhi ya nyota wake unaweza usiwe wa kwake kuufanya kwasababu anataka kusikiliza na mawazo ya wengine. Kipigo cha mabao 2-1 walichopata Chelsea kutoka kwa Sunderland mwishoni mwa wiki iliyopita kinamaanisha hata kama wakishinda mchezo wa Anfield inaweza isitoshe kuizuia Liverpool kushinda taji la ligi baada ya kupita miaka 24.

No comments:

Post a Comment