Tuesday, April 22, 2014

HATIMAYE UNITED WAMTIMUA MOYES RASMI.

HATIMAYE klabu ya Manchester United imemtupia virago meneja wake David Moyes baada ya wamiliki wake familia ya Glazer kumchoka kocha huyo raia wa Scotland. Moyes mwenye umri wa miaka 50, ambaye amejitengenezea rekodi zisizihitajika Old Trafford anakuwa meneja wa kwanza wa United kutimuliwa toka Ron Atkinson mwaka 1986. Klabu hiyo ilitangaza kumtimua Moyes katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter ambapo pia walimshukuru kwa juhudi zake katika kipindi chote cha miezi 10 alichoinoa timu hiyo. Moyes alichaguliwa na Sir Alex Ferguson kuchukua nafasi yake wakati kocha huyo alipostaafu msimu uliopita baada ya kuinoa timu hiyo kwa misimu 26. Mkongwe Ryan Giggs atachukua mikoba kama kocha wa muda wakati klabu ikitafuta mbadala wa Moyes, ambapo majina kama Jurgen Klopp, Louis van Gaal na Carlo Ancelotti yanapewa nafasi ya kuziba pengo hilo.

No comments:

Post a Comment