Tuesday, April 22, 2014

KIINGILIO CHA CHINI TAIFA STARS NA BURUNDI 5,000.

SHIRIKISHO la Soka nchini-TFF limetaja viingilio vya mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya Taifa Stars na timu ya taifa ya Burundi unaotarajiwa kuchezwa Aprili 26 mwaka katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Katika taarifa iliyotumwa katika vyombo vya habari na Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura, imedai kuwa mchezo utakuwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Taarifa hiyo iliendelea kudai kuwa kiingilio cha chini katika mchezo huo kitakuwa shilingi 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani wakati VIP A kiingilio kitakuwa 20,000 huku VIP B na C kiingilio kitakuwa 10,000. Taifa Stars kwasasa wako kambini katika hoteli ya Kunduchi Beach tayari kujiandaa na mchezo huo huku wapinzani wao Brundi wakiwa wametua nchini leo kwa ajili ya mechi hiyo ya kusisimua.

No comments:

Post a Comment