Tuesday, April 22, 2014

DORTMUND HAITAYUMBA KWA KUONDOKA KWA LEWANDOWSKI - WATZKE.

OFISA mkuu wa klabu ya Borussia Dortmund, Hans-Joachim Watzke amedai kuwa meneja Jurgen Klopp atahakikisha timu hiyo haitetereki kutokana na pengo la kuondoka kwa Robert Lewandowski. Nyota huyo wa kimataifa wa Poland ambaye alifikisha mabao 100 katika klabu hiyo kwenye mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Ujerumani dhidi ya Wolfsburg, atajiunga na Bayern Munich kwa uhamisho huru mwishoni mwa msimu huu. Hata hivyo, pamoja na kuondoka kwa mshambuliaji huyo, Watzke anaamini kuwa timu hiyo haitayumba kwani Klopp mara zote amekuwa akitafuta njia mbadala pindi anapoondokewa na nyota wake kama ilivyokuwa kwa Nuri Sahin aliyekwenda Real Madrid na Shinji Kagawa aliyekwenda Manchester United. Bosi huyo amesema anajua hawawezi kuziba la Lewandowski kama yeye lakini anajua pia hawawezi kuyumba kwasababu ya kuondoka kwake.

No comments:

Post a Comment