Tuesday, April 22, 2014

VAN GAALA APEWA NAFASI YA KUCHUKUA MIKOBA YA MOYES BAADA YA KLOPP KUCHOMOA.

KOCHA wa timu ya taifa ya Uholanzi, Louis van Gaal ameonyesha nia ya kutaka kuchukua mikoba ya David Moyes kama meneja mpya wa Manchester United. Mholanzi huyo aliwatonya marafiki zake kuwa anatamani kutua Old Trafford wakati mkataba wake wa kuinoa nchi hiyo utakapomalizika baada ya michuano ya Kombe la Dunia. Kumekuwa na ripoti zilizodai kuwa Van Gaal alikutana na ujumbe wa United wiki iliyopita na mazungumzo zaidi yanatarajiwa kuendelea wakati United itakapoanza hatua ya kutafuta mbadala wa Moyes. Jurgen Klopp pia aifuatwa na United lakini meneja huyo wa Borussia Dortmund alitangaza kutokuwa na mpango wa kuinoa United mapema leo. Klopp alikaririwa akidai kuwa United ni klabu kubwa na anajiona kuwa karibu na mashabiki wake lakini hawezi kuondoka Dortmund kwasasa.

No comments:

Post a Comment