Wednesday, April 23, 2014

TERRY, CECH WASHINDWA KUMALIZIA MSIMU.

NAHODHA wa Chelsea John Terry na golikipa Petr Cech wanatarajiwa kukosa mechi za Ligi Kuu zilizosalia baada ya kupata majeruhi katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Atletico Madrid jana. Terry alitolewa nje kwa matatizo ya mguu wakati Cech yeye alijumiza bega lake katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya bila kufungana. Meneja wa Chelsea, Jose Mourinho amesema Terry anaweza kucheza tena kama timu hiyo itafanikiwa kutinga fainali ya michuano hiyo itakayofanyika Mei 24 mwaka huu. Ligi Kuu nchini Uingereza inatarajiwa kufunga pazia lake Mei 11 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment