Wednesday, April 23, 2014

FERGUSON ALIKUWEMO KATIKA KIKAO CHA KUMTIMUA MOYES.

MENEJA wa zamani wa Manchester United, Sir Alex Ferguson anatarajiwa kuwa sehemu muhimu katika kutafuta mbadala wa David Moyes katika timu hiyo. Safari hii Ferguson aakuwa sambamba na wajumbe wote wa bodi ya klabu hiyo katika uchaguzi wa kocha mpya. Bodi hiyo ilikutana baada ya kipigo cha mabao 2-0 kutoka Everton Jumapili iliyopita kuzungumzia hatua ya kumfukuza Moyes na Ferguson pamoja na nguli wa zamani wa klabu hiyo Sir Bobby Charlton inaaminika walikuwemo katika kikao hicho. Ryan Giggs ndio aliyepewa mikoba ya kuinoa United kwa muda mpaka atakapopatikana kocha mpya lakini inaaminika kuwa mkongwe huyo hayupo katika orodha ya makocha watakaofanyiwa usaili.

No comments:

Post a Comment