Wednesday, April 23, 2014

MBINU CHAFU ZA MOURINHO ZAMKERA SUAREZ.

KIUNGO wa klabu ya Atletico Madrid, Mario Suarez ameeleza kuchukukizwa kwake na mbinu zisizo sahihi zilizokuwa zikitumiwa na Chelsea katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baina ya timu hizo. Suarez amesema anadhani wakongwe hao wa Ligi Kuu nchini Uingereza walikwenda katika Uwanja wa Vicente Calderon kwa dhumuni moja la kutafuta sare. Atletico wanaonolewa na Diego Simeone walimiliki mpira sehemu kubwa ya mchezo huo uliochezwa jana usiku lakini walishindwa kuipenya safu ya ulinzi ya Chelsea hivyo kusababisha timu hizo kutoka sare ya bila kufungana. Kiungo huyo amesema Chelsea wamepata walichokuwa wakikitaka yaani sare lakini bado wana mchezo wa marudiano hivyo anadhani bado wana nafasi.

No comments:

Post a Comment