Wednesday, April 23, 2014

KUFUZU LIGI YA MABINGWA ULAYA ITATUSAIDIA KATIKA USAJILI - AYRE.

MKURUGENZI mtendaji wa Liverpool, Ian Ayre amesema kufuzu kwa klabu hiyo katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kutawasaidia sana katika usajili majira ya kiangazi. Ushindi wa mabao 3-2 waliopata Liverpool dhidi ya Norwich City Jumapili iliyopita, umeithibitishia timu hiyo kumaliza katika nafasi tatu za juu na kuwafanya kurejea katika michuano hiyo toka mwaka 2009. Ayre amekiri timu kushindwa kufuzu michuano hiyo kipindi cha nyuma ilikuwa inawapa wakati mgumu kuzungumza na wachezaji. Bosi huyo amesema kipindi cha usajili hali ilikuwa ngumu akitolea mfano wlaipopata tabu kumshawishi Luis Suarez kubaki Liverpool kwasababu alikuwa akitaka kucheza katika michuano hiyo dhidi ya wachezaji bora. Lakini kwa mafanikio waliyopata safari hii ya kufuzu michuano hiyo huku wakiwa katika nafasi nzuri ya kunyakuwa taji la ligi kwa mara ya kwanza toka mwaka 1990, Ayre anaamini mazungumzo katika kipindi cha usajili yatakuwa rahisi kutokana na nafasi waliyonayo.

No comments:

Post a Comment