Monday, April 28, 2014

KUMPA GIGGS KIBARUA CHA KUINOA UNITED NI SAWA NA KUCHEZA KAMARI - BERG.

BEKI wa zamani wa Manchester United, Henning Berg anaamini itakuwa ni sawa na kucheza kamari kumteua Ryan Giggs kama meneja wa kudumu wa klabu hiyo. Kufuatia kutimuliwa kwa David Moyes Jumanne iliyopita, Giggs mwenye umri wa miaka 40 amekuwa akishikilia kwa muda kibarua hicho mpaka mwishoni mwa msimu, wakati Louis van Gaal akiaminika kukubali kutua Old Trafford baada ya mkataba wake na timu ya taifa ya Uholanzi kumalizika kiangazi hiki baada ya Kombe la Dunia. Giggs katika mechi yake ya kwanza ameiongoza United kuichabanga Norwich kwa mabao 4-0 mwishoni mwa wiki iliyopita lakini Berg anaamini nguli huyo bado anahitaji kocha mzoefu ili aweze kumsaidia. Berg amesema anaamini Giggs anaweza kuwa meneja mzuri huko mbele lakini kwasasa hana uzoefu anahitaji mtu mwenye uzoefu aweze kumsaidia.

No comments:

Post a Comment