Monday, April 28, 2014

SUAREZ, HAZARD WAZIKWAA TUZO UINGEREZA.

MSHAMBULIAJI nyota wa Liverpool, Luis Suarez ametunukiwa tuzo ya kuwa mchezaji bora wa mwaka nchini Uingereza katika sherehe zilizofanyika jijini London jana. Nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay, mwenye umri wa miaka 27 alisafiri kuelekea kwenye sherehe hizo baada ya Liverpool kupokea kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Chelsea mapema jana. Akihojiwa mara baada kukabidhiwa tuzo hiyo, Suarez amesema Ligi Kuu imejaa wachezaji wengi bora hivyo ni heshima kubwa kwake kwa wachezaji hao kukumbuka mchango wake ndani ya uwanja. Nyota wa Chelsea Eden Hazard yeye alichaguliwa kuwa mchezaji bora chipukizi wa mwaka katika tuzo hizo ambazo huandaliwa na Chama cha Wachezaji wa Kulipwa nchini Uingereza.

No comments:

Post a Comment