Friday, April 25, 2014

NAJIVUNIA KUINOA UNITED - GIGGS.

KOCHA wa muda wa klabu ya Manchester United, Ryan Giggs amesema kuifundisha timu hiyo ni moja ya matukio ya kujivunia katika maisha yake. Giggs raia wa Wales mwenye umri wa miaka 40 anategemewa kuingoza klabu hiyo katika mechi nne zilizobakia baada ya David Moyes kutimuliwa. Giggs ambaye ametumia maisha yake yote ya kucheza soka na sasa kocha wa muda akiwa na timu hiyo, anataka kuihakikishia klabu hiyo nafasi ya kushiriki michuano ya Europa League msimu ujao ambayo kwasasa inashikilia nafasi ya saba katika msimamo wa ligi. Akihojiwa katika mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari akiwa kocha leo, Giggs amesema anajisikia fahari na furaha kuifundisha klabu hiyo aliyoitumikia toka akiwa kijana mdogo.

No comments:

Post a Comment