Friday, April 25, 2014

SCOLARI ADOKEZA KIKOSI CHAKE.

KOCHA wa timu ya taifa ya Brazil, Luiz Felipe Scolari amemuongeza Thiago Silva, David Luiz na Fred katika orodha yake ndogo ya wachezaji atakaowajumuisha katika kikosi chake cha Kombe la Dunia. Brazil inatarajiwa kuanza kampeni zake za kutafuta taji lake la sita wakati michuano hiyo takaporejea nchini humo katika majira ya kiangazi mwaka huu. Scolari amesema Silva, Luiz na Fred wana uhakika wa kuwepo katika kikosi chake cha kitakachokuwa na wachezaji 23. Kocha huyo amesema hao ndio wachezaji wake viongozi na tayari ameshazungumza nao zaidi katika safari zao, hana shaka kuhusu orodha yake ya mwisho lakini atasubiri mpaka mwishoni mwa msimu ligi zitakapomalizika. Scolari anatarajia kuteua kikosi kamili kwa ajili ya michuano hiyo Mei 7 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment