Friday, April 25, 2014

RWANDA KUANDAA KAGAME, CHALENJI WAPEWA ETHIOPIA.

BARAZA la Michezo la Nchi za Afrika Mashariki na Kati-CECAFA limeiteua Rwanda kuwa mwenyeji wa michuano ya Kombe la Kagame itakayofanyika Agosti mwaka huu wakati Ethiopia wenyewe wameteuliwa kuandaa michuano ya Chalenji inayotarajiw akufanyika kati ya Novemba na Desemba. Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye amesema kuwa wameichagua Rwanda kuwa mwenyeji wa michuano hiyo ili kuadhimisha pamoja nao miaka 20 ya mauaji ya kimbari. Katika michuano ya mwaka jana klabu ya Vital’O ya Burundi ndio walikuwa mabingwa wa michuano hiyo iliyofanyika huko Darfur, Sudan. Yanga waliokuwa mabingwa wa michuano hiyo mwaka 2012 walishindwa kutetea taji lao mwaka jana baada ya kuamua kujitoa sambamba na Simba kutokana na masuala ya kiusalama nchini Sudan.

No comments:

Post a Comment