Friday, April 25, 2014

FA YATUMA MAOMBI YA WEMBLEY KUWA MWENYEJI WA EURO 2020.

CHAMA cha Soka nchini Uingereza-FA kimepeleka maombi ya Uwanja wa Wembley kuwa mwenyeji wa aidha nusu fainali na fainali ya michuano ya Euro 2020 au baadhi ya mechi za makundi. Maombi hayo yametumwa katika dakika za mwisho kabla ya muda wa mwisho kufanya hivyo wakati Wales na Scotland pia zimeomba uenyeji wa mechi za makundi. Ilitangazwa Desemba mwaka jana kuwa michuano hiyo ya Ulaya inatarajiwa kuandaliwa na miji mbalimbali kuzunguka bara hilo. Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA linatarajia kutangaza miji 13 itakayokuwa mwenyeji wa michuano hiyo katika sherehe zitakazofanyika Septemba 19 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment