Thursday, April 24, 2014

BELUSCONI AGOMA KUUZA AC MILAN.

MAOFISA wa AC Milan wamebainisha kuwa hakuna mpango wa kuuza klabu hiyo, pamoja na tetesi ya kutaka kununuliwa na mfanyabiashara wa Singapore Peter Lim. Vyombo vya habari nchini Italia vimedai kuwa bilionea huyo mwekezaji ametoa ofa ya euro milioni 500 kwa ajili ya kununua hisa nyingi za klabu hiyo. Mbali na Lim, kuna taarifa zingine zinazodai kuwa mfanyabiashara mwingine kutoka China Zong Qinghou pia anaangalia uwezekano wa kuinunua timu hiyo. Hata hivyo, mwenyekiti wa klabu hiyo Silvio Belusconi alikanusha tetesi hizo na kudai kuwa hana mpango kuachia umiliki kwenda kwa yoyote. Belusconi ndio anaemiliki hisa nyingi katika klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment