Thursday, April 24, 2014

STURRIDGE FITI KUIVAA CHELSEA.

MSHAMBULIAJI wa Liverpool, Daniel Sturridge anategemewa kurejea kutoka katika majeruhi katika mchezo wa Jumapili ambao watakwaana na Chelsea. Nyota huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye miaka 24 alikuwa akilalamika maumivu ya msuli katika ushindi wa mabao 3-2 waliopata dhidi ya Manchester City Aprili 13 hivyo kupelekea kutolewa nje. Toka apate majeruhi hayo alikosa mechi moja lakini sasa anategemewa kurejea tena uwanjani kuisaidia Liverpool katika mchezo huo muhimu ambao kama wakishinda utawafanya kuendelea kujikita kileleni hivyo kuweka hai matumaini yao ya ubingwa wa Ligi Kuu. Sturridge amesema kwasasa anajisikia vyema na ni mategemeo yake atakuwepo katika mchezo huo wa Jumapili lakini itategemea kama kocha Brendan Rodgers atamchagua.

No comments:

Post a Comment