Monday, April 28, 2014

NYOTA TISA HATARINI KUKOSA FAINALI YA LIGI YA MABINGWA ULAYA.

JUMLA ya wachezaji tisa wako hatarini kukosa mchezo wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kutokana na kuwa na kadi za njano kuelekea katika mchezo wa mkondo wa pili wa michuano hiyo. Kwa upande wa mabingwa watetezi Bayern Munich, mshambuliaji wao Mario Mandzukic yuko hatarini kufungiwa kucheza fainali ya michuano hiyo wakati watakapojitupa uwanjani kesho kujaribu kubadilisha matokeo ya kufungwa bao 1-0 na Real Madrid katika mchezo wa kwanza. Madrid wenyewe wana wachezaji watatu ambao wanaweza kukosa fainali hiyo itakayofanyika jijini Lisbon kama wakipewa kadi za njano katika mchezo huo utakaofanyika Ujerumani ambao ni Sergio Ramos, Xabi Alonso na Asier Illarramendi. Chelsea itaikaribisa Atletico Madrid katika mchezo wa maruadiano huku nyota wake wawili wa Kibrazil David Luiz na Willian wote wakiwa katika hatari kama hiyo ya kufugiwa mechi moja kama wakipewa kadi za njano katika mchezo huo. Atletico kama ilivyo kwa mahasimu wao Madrid nao wana wachezaji watatu waliokuwepo katika hatari hiyo ambao ni mabeki Emiliano Insua na Juanfran pamoja na kiungo Koke huku nahodha wao Gabi akiukosa mchezo wa marudiano kutokana na kuwa na kadi mbili za njano tayari.

No comments:

Post a Comment