Monday, April 28, 2014

NEYMAR AAPA KUPAMBANA NA UBAGUZI WA RANGI.

MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Neymar ameapa kupambana na unyanyasaji wa kibaguzi baada ya mchezaji mwenzake Dani Alves kutupiwa ndizi wakati wa mchezo wa La Liga dhidi ya Villarreal ambao walishinda maba 3-2 Jana. Beki huyo wa kimataifa wa Brazil alichukulia tukio hilo kwa utulivu kwa kuchukua ndizi hiyo aliyorushiwa na kuila lakini Neymar alitumia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram kukemea tukio hilo. Neymar aliandika katika katika mtadao wake huo kuwa watu wote ni sawa, wote ni nyani kemea ubaguzi wa rangi. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa ni aibu kwa karne hii watu kuendelea na vitendo hivyo, ni wakati wa watu kupaza sauti na kukemea udhalilishaji huo.

No comments:

Post a Comment