Monday, April 28, 2014

DEL PIERO AAMUA KUTUNDIKA DARUGA.

MCHEZAJI mkongwe Alessandro Del Piero ameamua kutundika daruga kuitumikia klabu ya Sydney FC lakini anaweza kurejea kwa shughuli nyingine. Nguli huyo wa zamani wa Juventus amekuwa akihusishwa na tetesi za kuwa kocha katika klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu nchiniAustralia maarufu kama A-League baada ya Frank Farina kutimuliwa. Del Piero mwenye umri wa miaka 39 na klabu hiyo wanataka kuendelea na mahusiano lakini haijabainika wazi ni uhusiano wa namna gani. Baada ya kufunga mabao 24 ambayo yamemfanya kumaliza kama mfungaji bora wa klabu katika misimu yote miwili aliyoitumikia, Del Pierro ametoa ujumbe wa kushukuru na kuaga katikamtandao wake. Del Piero amesema katika ujumbe huo ule wakati umewadia safari yake akiwa na Sydney FC inakaribia ukingoni ingawa inasikitisha lakini amekuwa na muda mzuri katika kipindi chote alichoitumikia.

No comments:

Post a Comment