Monday, April 28, 2014

WACHEZAJI WA LOS ANGELES CLIPPERS WAFANYA MAANDAMANO YA KIMYA KIMYA KUFUATIA KAULI YA KIBAGUZI YA BOSI WAO.

WACHEZAJI wa mpira wa kikapu nchini Marekani wamefanya maandamano ya kimya kimya kufuatia ripoti kuwa mmiliki wa timu yao amerekodiwa kisiri akitoa kauli za kibaguzi. Los Angeles Clippers waliingia kupasha misuli moto jana huku fulana zao wakiwa wamezigeuza ndani-nje ili kuficha nembo ya timu hiyo. Chama cha Mpira wa Kikapu nchini Marekani-NBA kinachunguza taarifa hiyo iliyotolewa na mtandao wa habari za mastaa wa TMZ kuwa mmiliki wa Clippers Donald Sterling ndio aliyetoa kauli hiyo. 
Wachezaji wa timu hiyo walivaa vita vyeusi mikononi huku wote wakivaa soksi nyeusi katika jezi zao za kawaida. Sterling aliinua Clippers mwaka 1981 na hakuwepo katika mchezo huo dhidi ya Golden State Warriors uliofanyika jijini Oakland ambao wachezaji wake walifanya mgomo huo wa kimya kimya.

No comments:

Post a Comment