Tuesday, April 22, 2014

SIKUPENDA KUPANGWA NA REAAL MADRID - MARTINEZ.

KIUNGO wa klabu ya Bayern Munich, Javi Martinez amekiri hakutaka timu yake ipangwe kuchuana na Real Madrid katika hatua ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Mabingwa hao watetezi wa michuano hiyo wanatarajiwa kupepetana na Madrid katika mchezo wa mkondo wa kwanza utakaochezwa kesho ambao utakuwa ni kama marudiano ya nusu fainali ya mwaka 2012 ambayo Bayern walivuka kwa changamoto ya mikwaju ya penati. Martinez anaamini kuwa Madrid ni timu ngumu pekee iliyobakia katika michuano hiyo ambayo itabidi wapambane nayo na kuwaonya wachezaji wenzake kuwa makini kama wanataka kutetea taji lao. KIungo aliendelea kudai kuwa Madrid ni timu ambayo inakuwa siku hadi siku huku wakiwa na wachezaji nyota kama Angel Di Maria, Gareth Bale na Cristiano Ronaldo ambao wanaweza kuleta madhara wakati wowote unapocheza nao.

No comments:

Post a Comment