Tuesday, April 22, 2014

ETO'O KUIKOSA ATLETICO MADRID.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Chelsea Samuel Eto’o anatarajiwa kuukosa mchezo wa mkondo wa kwanza wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhhidi ya Atletico Madrid kutokana na majeruhi ya goti. Nyota huyo ameshindwa kusafiri na kikosi cha timu hiyo kilichoelekea nchini Hispania kwa ajili ya mchezo na vinara hao wa La Liga utakaochezwa baadae leo. Eto’o aliifungia bao Chelsea wakati ilipokubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Sunderland Jumamosi iliyopita lakini alitolewa baada ya dakika 74 za mchezo. Hata hivyo, Eden Hazard ameanza mazoezi kufuatia majeruhi yaliyokuwa yakimsumbua na kumfanya kukaa nje kwa wiki mbili. Kukosekana kwa Eto’o, Mourinho anaweza kumchagua Fernando Torres ambaye aliondoka Atletico mwaka 2007 kujiunga na Liverpool kuziba nafasi hiyo.

No comments:

Post a Comment